Beda Mheshimiwa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Beda maarufu kama Mheshimiwa tangu enzi za uhai wake (Wearmouth-Jarrow, Northumbria, leo nchini Uingereza, 672 au 673 – 25 Mei - Wearmouth-Jarrow, 735) alikuwa mmonaki, padri, mwanateolojia na mwanahistoria nchini Uingereza.
Mtumishi wa Kristo monasterini tangu umri wa miaka minane hadi kifo chake, alitumia maisha yake yote kutafakari na kufafanua Biblia; pamoja na kushika kila siku nidhamu ya kimonaki na kumuimbia Mungu kanisani, alipenda daima kujifunza, kufundisha na kuandika.
Hasa anafahamika kwa kitabu chake “Historia ya kikanisa ya taifa la Waingereza” (kwa Kilatini: Historia ecclesiastica gentis Anglorum). Akiona Kanisa lilivyozidi kustawi kati ya mataifa mapya, alipenda kuonyesha lisivyobanwa na ustaarabu mmoja, bali linakumbatia kila aina ya utamaduni ili kuikamilisha katika Kristo.
Beda alichangia kwa kiasi kikubwa uenezaji wa hesabu ya miaka baada ya Kristo kuzaliwa.
Mwaka 1899 alitangazwa na Papa Leo XIII kuwa mtakatifu na mwalimu wa Kanisa.