Tausi
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tausi ni ndege wakubwa wa jenasi Pavo na Afropavo katika familia ya Phasianidae.
Dume ana rangi ing’aayo ya majani au buluu na mkia wake ni mrefu mwenye rangi nyingi. Jike ana rangi inayofifia pengine kahawia tu. Jinsia zote zina ushungi. Dume hukoga mkia kwa ubembelezi.
Hula matunda, maua, wadudu na watambazi. Hutaga mayai matatu hadi manane ardhini.
Tausi wa Kongo anatokea Kongo ya Kidemokrasia. Spishi mbili nyingine zinatokea misitu ya Asia, lakini zimewasilishwa katika sehemu nyingine za dunia, hususa tausi mhindi.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.