From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtagusano sumakuumeme (ing. electromagnetic force au electromagnetic interaction) ni moja kati ya kani msingi wa ulimwengu.
Mtagusano huu unasababisha mambo mengi tunayoyaona kila siku kama vile nuru, umeme na usumaku. Ni kani ya kimsingi pia kwa kuamulia tabia za molekuli na atomi.
Jina la "sumakuumeme" ni tafsiri ya gir. / ing. "electromagnetic" inayotokana na maneno ya Kigiriki ἢλεκτρον, ēlektron (kaharabu[1]) na μαγνήτης, magnetis (sumaku).
Umeme na usumaku ni nyuso mbili za jambo lilelile.
Kwa karne nyingi wataalamu waliona umeme na usumaku ni kani mbili tofauti. Tangu mwanzo wa karne ya 19 wanasayansi walitambua uhusiano wa karibu kati ya hizi mbili.
Hans Christian Ørsted aliona mwaka 1820 ya kwamba kutirikika kwa chaji ya umeme katika waya kunavuta sindano ya sumaku na hivyo kunaunda uga wa sumaku.
Wengine waliendelea kujenga juu ya matokeo yake na Mskoti James Clerk Maxwell alieleza misingi ya nadharia ya uga wa sumakuumeme katika hesabu inayoitwa milinganyo ya Maxwell. Alifaulu kuunganisha maelezo kwa ajili ya umeme, usumaku na elimumaonzi kuwa pande mbalimbali za kitu kilekile, yaani uga wa sumakuumeme. Alitabiri kuwepo kwa mawimbi ya sumakuumeme na nuru kuwa umbo mojawapo la mawimbi haya.
1873 alitoa kitabu chake "Treatise on Electricity and Magnetism" (tasinifu kuhusu umeme na usumaku) alipojumlisha maelezo yake. Alionyesha kuwa kuathiriana kwa chaji hasi na chaji chanya kunasababishwa na kani 1 tu akaonyesha matokeo manne makuu kutokana na hii:
Hasa tokeo la mwisho lilikuwa msingi kwa kuanzisha mitambo ya kutengeneza umeme kwa mashine kama jenereta.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.