Saruji (pia: simiti, simenti) ni mata laini kama ungaunga unaotengenezwa kutokana na mawe chokaa, udongo wa mfinyanzi, mchanga, chuma na mengine. Kwa kawaida huonekana kama unga wa rangi ya kijivu.

Thumb
Kiwanda cha saruji

Hukorogwa na maji kuwa na hali kati ya ujiuji ila baada ya muda inaanza kuganda na kuwa imara kama jiwe.

Saruji imekuwa muhimu sana katika shughuli za ujenzi. Awali ilitumiwa kwa kushika mawe au matofali ya ukuta vikae pamoja.

Baadaye ikagunduliwa ya kwamba saruji ikichanganywa na mchanga ma mawe madogo (kama kokoto) kuwa zege inaweza kumwagwa kati ya bao mbili na kuwa imara ndani yake. Kwa njia hiyo imewezekana kujenga haraka sana kwa kumwaga mchanganyiko wa zege ya saruji katika nafasi zilizoandaliwa awali. Hapo nondo za chuma zinaingizwa ndani ya ukuta au sakafu ya saruji kwa kusudi la kuongeza uimara.

Viungo vya nje

Ukweli wa haraka
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Funga
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.