Nyota nova
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nyota nova (lat. stella nova kwa maana ya "nyota mpya", ing. nova) ni ongezeko la ghafla la mwangaza wa nyota. Ilhali idadi kubwa za nyota hazionekani kwa macho matupu ongezeko hili linatokea mara nyingi kama "nyota mpya" angani inayoweza kung'aa sana hata kushinda nyota zote nyingine. Hivyo inaonekana kwa muda tu na kupotea tena kwa mtazamaji asiye na darubini.
Zamani nyota zote zilizowaka hivi ziliitwa kwa jina lilelile "nova". Jina hili lilitumiwa mara ya kwanza na Tycho Brahe ambaye katika mwaka 1572 aliona nyota mpya katika eneo la kundinyota Mke wa Kurusi (Cassiopeia) na kueleza utafiti wake katika kitabu cha "De stella nova"(Kuhusu nyota mpya) [1]. Wakati huo Tycho Brahe alianzisha majadiliano kuhusu mafundisho ya wataalamu wa kale walioamini kwamba hakuna mabadiliko yoyote kwenye anga ya nyota[2].
Hata kabla ya Tycho kulikuwa na taarifa kuhusu nyota zilizotokea angani. Taarifa ya kale zaidi ni ya wanaastronomia nchini China kwenye mwaka 185 baada ya Kristo kuhusu "nyota geni" iliyoonekana karibu na Rijili Kantori (α Centauri). Nova nyingine ilitazamiwa mwaka 1054 na kurekodiwa na wanaastronomia Wachina, Wajapani na Wakristo wa Baghdad. Mabaki yake huonekana hadi leo kama "Nebula ya Kaa" katika eneo la Tauri (Taurus).
Tangu karne ya 20 vipimo na elimu iliyopanuka vilifanya wanaastronomia kutofautisha kati ya "nova" na "supanova" ambazo zote ni "nyota mpya" zinazotokea angani kwa muda ila kwa sababu tofauti.
Nyota nova za kawaida zinatokea katika mfumo wa nyota maradufu. Nadharia inayokubalika na wengi inasema: nyota kibete cheupe na nyota kubwa, hasa jitu jekundu, zinazungukana kwa umbali wa karibu. Kibete cheupe kimeshamaliza hidrojeni yake na kujikaza, hivyo graviti yake bado ni kubwa ingawa mjao wake ni mdogo, pia ina joto. Jitu jekundu la jirani linaendelea kupanuka. Hapa sehemu ya mata ya tabaka za nje ya nyota kubwa inavutwa na graviti ya nyota ndogo na kuhamia upande wake. Sehemu ya mata hii ni hidrojeni inayokusanyika kwa umbo la diski ya uongezekaji[3] inayozunguka Kibete Cheupe na hatimaye kufikia karibu zaidi na kuunda angahewa. Hidrojeni hii inapashwa moto na uso wa Kibete Cheupe hadi kufikia halijoto ya kutosha ya kuanzisha myeyungano wa kinyuklia (nuclear fusion).
Mchakato huu unazalisha kiasi kikubwa cha nishati na kurusha sehemu ya hidrojeni inayowaka kwenye anga ya nje. Hii inaongeza mwangaza wa nyota inayoonekana sasa kama nyota nova. Kiasi cha masi inayorushwa angani wakati wa kuwaka inalingana takriban na 1/10,000 ya masi ya Jua.
Maendeleo ya nova inafuata hatua kama hizi:
Kila mwaka kuna takriban nyota nova 10 zinazotazamwa katika Njia Nyeupe[4]. Lakini wanaastronomia hukadiria kwamba idadi halisi ni kubwa zaidi, labda takribani 50 zinazotokea kila mwaka katika galaksi yetu[5].
Nyota nova zinagunduliwa pia katika galaksi nyingine, kwa mfano katika galaksi ya Andromeda (M31) na penginepo[6].
Kinadharia mchakato huu unaweza kurudia mara kadhaa kwa sababu baada ya mlipuko wa angahewa ya nyota ndogo, mata kutoka jirani inaanza kuvutwa tena. Nyota RS Ophiuchi katika kundinyota ya Hawaa ilitazamwa kuwaka mara sita[7]: 1898, 1933, 1958, 1967, 1985 na 2006.
Hadi sasa kuna nyota nova 10 zilizotazamwa kuwaka tena kati ya takriban 400 zilizogunduliwa katika Njia Nyeupe[8]; kwa hiyo hakuna uhakika bado kuhusu muda wa kawaida uliopo baina ya kuwaka kwa nyota. Kama nyota kibete imeendelea kukusanya mata nyingi kuna uwezekano kwamba inalipuka mwishoni kama supanova [9]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.