From Wikipedia, the free encyclopedia
Jeni (pia kinasaba; kwa Kiingereza "gene", kutoka Kigiriki γόνος, gonos, yaani uzao) ni sehemu kwenye DNA. DNA ni mkusanyiko wa taarifa za kemikali ambazo hubeba maelekezo kwa ajili ya kutengeneza protini kwenye seli. Kila jeni au kinasaba hubeba habari zinazothibiti tabia za binadamu na kila kiumbehai (kama vile wanyama na mimea) zilizopokewa kutoka wazazi kama vile mwonekano, jinsia na maumbile yote.
Kila jeni ina seti moja ya maelekezo. Maelekezo hayo kawaida ni msimbo wa protini fulani.
DNA ya binadamu huwa na jeni takribani 27,000. Nusu ya jeni ya mtu hutoka kwa mama. Nusu nyingine hutoka kwa baba.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.