Roboti ya viwandani (kwa Kiingereza: industrial robot) ni mfumo wa roboti unaotumika katika uzalishaji wa bidhaa. Roboti za viwandani ni za kiotomatiki, zinaweza kupangwa na zinaweza kusonga kwa ekseli tatu au zaidi.

Thumb
Seti ya roboti za ekseli sita zinazotumika kuchomelea.

Roboti za viwandani hutumiwa kwa shughuli kama kuchomelea vyuma, kupaka rangi, kuunganisha na kutenganisha, [1] kuchukua na kuweka vipuli kwa bodi za saketi zilizochapishwa, kuweka lebo, ukaguzi wa bidhaa na majaribio; yote yametimizwa kwa kasi, na usahihi. Zinaweza kusaidia katika utunzaji wa nyenzo.

Katika mwaka wa 2020, roboti za viwandani milioni 1.64 zilikuwa zikifanya kazi kote ulimwenguni kulingana na Shirikisho la Kimataifa la Roboti (IFR). [2]

Marejeo

Viungo vya nje

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.