Kasoko ya dharuba (kwa Kiingereza impact crater) ni uwazi kwenye ardhi unaotokana na mshtuko wa kugongwa na gimba. Kasoko ina umbo la duara; katikati ni kama shimo na ukingo wake unainuka juu ya uwiano wa mazingira yake. Duniani kasoko zinapatikana mara nyingi kutokana na milipuko ya volkeno au milipuko mingine.

Thumb
Kutokea kwa kasoko ya dharuba
Kutokea kwa kasoko kutokana na dharuba (filamu ya maabara ya NASA)

Katika magimba ya angani yenye uso thabiti kuna kasoko nyingi kama matokeo ya kugongwa na magimba kutoka anga-nje. Kwa mfano, kwenye Mwezi wa Dunia kuna kasoko nyingi zilizosababishwa na migongano ya asteroidi au vimondo. Pigo la kitu kigumu linarusha mata iliyopo mahali pa mgongano ikae pembeni kwa shimo hilo kwa umbo la ukingo wa mviringo.

Duniani kasoko nyingi kutokana na mishtuko ya aina hiyo zinasawazishwa baada ya muda fulani kutokana na mmomonyoko unaosababishwa na mvua na upepo; kwenye magimba pasipo angahewa kama Mwezini zinabaki kwa miaka milioni kadhaa.

Tazama pia

Tanbihi

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.