From Wikipedia, the free encyclopedia
Maandishi madogo
ISO 216 ni orodha ya vipimo sanifu iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Usanifishaji (ISO) kwa ajili ya fomati za karatasi. Orodha hii inafafanua fomati za karatasi za aina "A" na "B" pamoja na A4 ambayo ni ukubwa unaotumiwa zaidi duniani. Zinatumiwa kote duniani isipokuwa Marekani bado wanatumia fomati tofauti.
Fomati zote za ISO 216 (na vipimo vya kuambatana nayo ISO 217 na ISO 269) vinafuata uhusiano wa 1: kati ya upande mrefu na upande mfupi. Faida yake ni ukikunja karatasi hizi kwa nusu yake, hata sehemu hizi zitakuwa tena na uhusiano huohuo baina ya upande ndefu na fupi. Pia eneo la kila fomati ni nusu ya eneo la fomati kubwa zaidi.
Fomati ya kimataifa ya ISO 216 inafuata utaratibu uliofafanuliwa nchini Ujerumani tangu mwaka 1922 kwa jina la DIN 476.
Fomati za A | Fomati za B | Fomati za C | |||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
A0 | 841 × 1189 | B0 | 1000 × 1414 | C0 | 917 × 1297 | ||||
A1 | 594 × 841 | B1 | 707 × 1000 | C1 | 648 × 917 | ||||
A2 | 420 × 594 | B2 | 500 × 707 | C2 | 458 × 648 | ||||
A3 | 297 × 420 | B3 | 353 × 500 | C3 | 324 × 458 | ||||
A4 | 210 × 297 | B4 | 250 × 353 | C4 | 229 × 324 | ||||
A5 | 148 × 210 | B5 | 176 × 250 | C5 | 162 × 229 | ||||
A6 | 105 × 148 | B6 | 125 × 176 | C6 | 114 × 162 | ||||
A7 | 74 × 105 | B7 | 88 × 125 | C7 | 81 × 114 | ||||
A8 | 52 × 74 | B8 | 62 × 88 | C8 | 57 × 81 | ||||
A9 | 37 × 52 | B9 | 44 × 62 | C9 | 40 × 57 | ||||
A10 | 26 × 37 | B10 | 31 × 44 | C10 | 28 × 40 |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.