Dawati (kutoka neno la Kiarabu; pia deski[1] kutoka neno la Kiingereza desk) ni meza inayotumiwa hasa na mwanafunzi kwa kuandikia au kusomea mara nyingi ikiwa na sanduku la kuwekea vitabu, madaftari na kalamu.

Thumb
Madawati darasani nchini Madagaska
Thumb
Dawati la shule kwenye makumbusho nchini Norwei.

Madawati ya shule mara nyingi hutengenezwa pamoja na kiti chake kama kipande kimoja, ilhali kimo cha sehemu ya meza na ya kiti hulingana na umri wa wanafunzi wanaolengwa. Upana wa dawati hutengenezwa kulingana na idadi ya watu wanaokaa katika dawati hilo. Kuna dawati la mtu mmoja watu wawili na watu watatu.

Madawati hupatikana shuleni, ofisini, nyumbani na kadhalika.

Wakati mwingine dawati linataja mtoto wa meza au saraka pekee.

Kwa maana tofauti kidogo "dawati" linaweza kumaanisha pia ofisi, kitengo au idara ndani ya taasisi fulani; kwa mfano "dawati la vijana" linaweza kutaja afisa au maafisa wanaohusika na mambo ya vijana katika ofisi kuu ya chama.

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.