From Wikipedia, the free encyclopedia
Desibel (kutoka Kiingereza: decibel; kifupi: dB) ni kizio cha upimaji wa nguvu au ukali. Kinalinganisha vipimo viwili kwa kutumia logi.
Matumizi yake ni hasa katika upimaji wa sauti na katika teknolojia ya umeme kwa kutaja kuongezeka au kupungua kwa volteji au sauti.
Kizio cha msingi ni "bel" na desibel ni sehemu yake ya kumi.
Nyongeza ya desibeli 3 inalingana takriban na kuzidisha nguvu mara mbili.
Kizio cha msingi cha bel kilipata jina lake kwa kumbukumbu ya Alexander Graham Bell aliyekuwa mmoja wa wabunifu wa simu.
Mara nyingi, desibeli hutumiwa kutaja ukubwa wa sauti kulingana na jinsi tunavyoisikia.
Decibel si kipimo sanifu cha SI.
Baadhi ya mifano ya sauti ni:
Kiwango cha Sauti | Mifano |
---|---|
171 dB | Karibu na bunduki kubwa ikipiga risasi |
150 dB | Karibu na injini ya ndege |
110-140 dB | Injini ya ndege kwa umbali wa mita 100 |
130-140 dB | Watu wengi huanza kuhisi maumivu |
130 dB | Baragumu (umbali wa nusu mita) |
120 dB | Tarumpeta ya Vuvuzela (kwa umbali wa mita 1), hatari ya uharibifu wa sikio |
80-90 dB | Trafiki kwenye barabara kuu |
60-80 dB | Gari la abiria |
40-60 dB | Mazungumzo ya kawaida |
20-30 dB | Chumba tulivu sana |
10 dB | Jani kung'aa, kupumua kwa utulivu |
0 dB | Sauti ndogo kabisa inayosikika karibu na sikio |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.