Bahati (kutoka neno la Kifarsi/Kiajemi "bakht", بخت; pia: sudi; kwa Kiingereza: lucky) inatafsiriwa kwa namna tofauti.

Thumb
Jani linalodhaniwa kuleta bahati njema.

Kwa mfano, Kamusi ya Noah Webster inafafanua bahati kama "nguvu isiyo na lengo, isiyotabirika na isiyotawalika inayosababisha matukio mazuri au mabaya kwa mtu binafsi au kundi la watu".[1]

Kumbe Max Gunther inatafsiri hivi: ni "matukio ambayo yanaathiri maisha ya mtu na yanaonekana kuwa nje ya udhibiti wake".[2]

Uwepo wa bahati unasadikiwa au kukanushwa kadiri ya utamaduni, falsafa, dini na hisia za watu. Kwa mfano Ukristo unafundisha Maongozi ya Mungu ambayo yanategemea Hekima yake, si bahati nasibu.

Tanbihi

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.