Simaki (ing. na lat. Arcturus ark-tu-rus, pia α Alpha Bootis, kifupi Alpha Boo, α Boo) ni nyota angavu zaidi katika kundinyota ya Bakari (Bootes). Ni pia nyota angavu ya nne kwenye anga la usiku. Mwangaza unaoonekana ni -0.05 mag.

Ukweli wa haraka
Simaki (Alfa Bootis, Arcturus)
Thumb
Kundinyota Bakari (Bootes)
Mwangaza unaonekana 0.05
Kundi la spektra K0 III
Paralaksi (mas) 88.83 ± 0.54
Mwangaza halisi 36.7
Masi M☉ 1.08
Nusukipenyo R☉ 25.4
Mng’aro L☉ 170
Jotoridi usoni wa nyota (K) 4286
Muda wa mzunguko siku 48
Majina mbadala α Boötis, 16 Boötes, BD+19°2777, GCTP 3242.00, GJ 541, HD 124897, HIP 69673, HR 5340, LHS 48, SAO 100944.
Funga
Thumb
Simaki (Arcturus) katika kundinyota yake ya Bakari – Bootes jinsi inavyoonekana kwa mtazamaji wa Afrika ya Mashariki
Thumb
Ulinganifu wa ukubwa baina ya Arcturus (Simaki) na Jua; hata hivyo masi halisi ya Simaki inafanana na Jua

Jina

Simaki ilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. [1]. Walipokea jina hili kutoka Waarabu wanaosema السماك الرامح as-simak ar-rami ambalo linamaanisha “mwenye kushika mkuki aliyeinuliwa juu”[2]. Hapa Waarabu walichagua hadithi kutoka kwa mitholojia ya Kigiriki iliyosimuliwa kuhusu kundinyota ya Bakari ambako masimulizi mbili tofauti zilichanganika. Hadithi ya mchunga au kuendesha ng’ombe ilikuwa msingi wa jina “Bakari” kwa kundinyota lakini “Mshika mkuki” inarejelea hadithi mbadala kuhusu mwindaji anayemfuata Dubu Mkubwa (kundinyota jirani) akishika mkuki wa kuwinda na kusindikizwa na Mbwa Wawindaji. Masimuliza haya hayapatikani kwa Ptolemaio katika kitabu chake cha Almagesti lakini yalishuhudiwa kati ya Wagiriki angalau tangu Hesiodo.

Katika matumizi ya kimataifa Umoja wa Kimataifa wa Astronomia ulichagua jina la Kigiriki "Arcturus" kwa maana "mchunga dubu"[3].

Tabia

Simaki - Arcturus ina mwangaza unaoonekana wa -0.05 mag na mwangaza halisi ni -0.30. Hivyo no nyota angavu ya nne baada ya Shira (Sirius) (Vmag −1.46), Suheli (Canopus) (Vmag −0.72) na Rijili Kantori (Alpha Centauri) (Vmag −0.27).

Simaki ni nyota ya karibu kiasi ikiwa umbali wake na Dunia ni miaka nuru 36.7 [4].

Masi yake ni M☉ 1.08 na nusukipenyo chake R☉ 25.4 (vizio vya kulinganisha na Jua letu) [5]. Ni nyota jitu jekundu katika kundi la spektra K0 III. Ilhali masi yake inalingana takriban na Jua letu kipenyo chake ni kubwa zaidi mara 25 na sababu yake ni ya kwamba jitu jekundu ni nyota iliyopanuka baada ya kuishia hidrojeni katika kitovu chake; katika hali hii kitovu cha nyota kinajikaza na myeyungano wa hidrojeni unahamia kwenye tabaka za nje za nyota. Hii inasababisha kupanuka kwa nyota na kuongezeka kwa mwangaza wake.

Kuna dalili ya kwamba Simaki ni nyota maradufu lakini hii haijathibitishwa bado. [6]

Tanbihi

Viungo vya Nje

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.