Aktini (actinium) ni elementi ya kikemia yenye namba atomia 89 na alama ya Ac . Uzani atomia wa Aktini ni 227.
Aktini (Aktinium) | |
---|---|
Jina la Elementi | Aktini (Aktinium) |
Alama | Ac |
Namba atomia | 89 |
Mfululizo safu | (haijulikani) |
Uzani atomia | 227 |
Valensi | 2, 8, 18, 32, 18, 9, 2 |
Densiti | 10 g/cm³ (kadirio) |
Ugumu (Mohs) | - |
Asilimia za ganda la dunia | 0 % (haba mno) |
Hali maada | mango |
Mengineyo | nururifu |
Aktini ni metali yenye rangi ya fedha. Ni nururifu kiasi cha kung'aa kwenye giza. Hata kiwango kidogo cha aktini ni hatari kwa afya ya watu. Isotopi zake huwa na nusumaisha ya siku chache, isipokuwa 227Ac, inayotokea kiasili katika madini ya urani, ina nusumaisha ya miaka 21.8.
Aktini iligunduliwa mnamo 1899 na Mfaransa André-Louis Debierne. Mnamo 1899, Debierne alielezea dutu hii kuwa inafanana na titani [1] na pia na thori . [2]
Marejeo
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.