From Wikipedia, the free encyclopedia
Wavuti wa Walimwengu (kifupi: WWW; pia: Wavuti; Kiingereza: World Wide Web), ni sehemu ya tovuti yenye wavuti nyingi. Sehemu nyingine za tovuti, kama huduma ya baruapepe (email) si sehemu ya WWW.
Tovuti za WWW zinafanywa na kurasa zenye matinikivo (hypertext) zinazoelekezana kwa njia ya viungokivo (hyperlinks). Yaliyomo ya wavuti hizo ni mara nyingi matini (text) pamoja na picha za mgando na za video, hati za sauti au muziki.
WWW ulianzishwa mwaka 1989 na Tim Berners-Lee kwenye taasisi ya CERN huko Geneva, Uswisi. Alitunga namna mpya ya ukurasa kwa kutumia lugha ya HTML. Alilenga kupata nafasi ya kubadilishana matokeo ya kazi yake na wataalamu wengine. Kwa maneno yake mwenyewe:
Mnamo Machi 1989 Berners-Lee alitumia kwa mradi wake jina la "Mesh" lililofutwa tena kwa sababu lilikuwa karibu mno na neno "mess" (=fujo). Baadaye alijaribu kutumia majina ya "Mine of Information" (ing. "Mgodi wa habari") au "The Information Mine" lakini vifupi vyao "MOI" (kwa Kifaransa "mimi") na TIM (jina lake mewenyewe) yalikuwa na harufu ya ubinafsi. Pia picha ya "mgodi" ilionekana haifai maana mgodi ni mahali pa kuchukulia kitu lakini wavuti ni pia mahali pa kupelekea habari, si kujipatia pekee. [1]
Hatimaye Berners-Lee alibuni majina ya "Web" ("utando") na "World Wide Web". Jina la "web" lilionekana kufaa vema kutokana na matumizi ya jina katika hisabati kwa wavu wa vinundu ambako kila kimoja kimeunganishwa na kingine.[2]
Berners Lee alibuni misingi mitatu kwa kuanzisha wawuti wa walimwengu:
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.