Ukoloni Mamboleo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ukoloni Mamboleo ni neno linalotumiwa na wakosoaji wa ukoloni kuelekezwa kwa nchi tajiri kuendelea kuingilia masuala ya nchi zinazoendelea baada ya ukoloni wenyewe kwisha kwa ukiukaji wa azimio la Umoja wa Mataifa. Wanakosoa mataifa ya kibepari kuhusika na dhuluma katika biashara ya kisasa na yaliyokuwa makoloni.
Wakosoaji wanasisitiza kwamba wafanyabiashara binafsi na makampuni ya biashara ya kigeni huendelea kunyonya rasilimali za mataifa baada ya enzi ya ukoloni kama ilivyotekelezwa kutoka karne ya 16 hadi karne ya 20.
Katika matumizi mapana, Ukoloni Mamboleo huweza kumaanisha ule ushiriki wa nchi zenye nguvu katika mambo ya nguvu chini ya nchi; hii ni muhimu hasa Amerika kusini.
Kwa maana hii, Ukoloni Mamboleo huweza kutaja aina ya kisasa ya ukoloni, uchumi wa ubeberu: kwamba mataifa yenye nguvu kuishi kama wakoloni, na tabia hii inafananishwa na ukoloni.