![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/17/Califate_750.jpg/640px-Califate_750.jpg&w=640&q=50)
Khalifa
cheo cha kifalme kulingana na madai ya kuwa mrithi wa Muhammad / From Wikipedia, the free encyclopedia
Khalifa, ni cheo cha kihistoria kwa ajili ya kiongozi wa umma (jumuiya ya Uislamu). Ni neno la Kiarabu خليفة khalīfah linalomaanisha "makamu". Khalifa ni kifupi chake cha خليفة رسول الله "khalifatu-rasul-i-llah" kinachomaanisha "Makamu wa mtume wa Allah/Mungu". Hivyo mana yake ni makamu au mfuasi wa Mtume Muhammad katika nafasi yake kama kiongozi wa Waislamu.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/17/Califate_750.jpg/640px-Califate_750.jpg)
Cheo cha khalifa kilitumiwa pamoja na cheo cha "amīr-al-mu'minīn" ( أمير المؤمنين ) "Jemadari Mkuu wa wenye Imani (=Waislamu)".
Utaratibu wa uongozi wa khalifa ulianzishwa baada ya kifo cha Mtume Muhammad mwaka 632 na kuishia 3 Machi 1924 katika mapinduzi ya Atatürk.