Timazi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Timazi ni kifaa cha ujenzi kinachosaidia kujenga ukuta kiwima-wima.
Kimsingi ni kitu kidogo na kizito kama jiwe, kipande cha metali ya risasi au chuma kilichofungwa kwa kamba. Uzito wa uzani utanyosha kamba kuwa nyoofu. Timazi ikitundikwa kando la ukuta inaelekea chini kiwima. Hapo kamba inatakiwa kwenda sambamba kabisa na ukuta. Baada ya kuweka timazi mjenzi anaona kama kuna tofauti au la. Picha naonyesha mfano wa ukuta wima (upande wa kushoto) na usio wima (upande wa kulia).
Katika ujenzi wa kisasa kuna mitambo inayochukua nafasi ya wima ya kawaida.