Ndezi
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ndezi ni wagugunaji wakubwa wa familia Thryonomyidae ambao wana mnasaba karibu kiasi na nungunungu. Wanatokea mahali panyevu pa Afrika kusini kwa Sahara. Wamo miongoni mwa wagugunaji kubwa kabisa duniani. Mwili wao una urefu wa sm 35-60 na uzito wa kg 6-10. Wana manyoya magumu yenye rangi ya kahawa na vidoa kijivu na njano. Hula manyasi ya maji porini lakini katika maeneo ya kilimo hula mimea ya shamba kama muwa, muhogo n.k. Wanaweza kudidimiza hasara kubwa. Ndezi hufugwa sana huko Benini na Togo, na hata nchini Kameruni, Kodivaa, Gaboni, Gana, Nijeria, Senegali na Kongo wakulima wahimizwa kufuga wanyama hawa. Nyama yao ni nzuri sana..
Ndezi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Ndezi mkubwa (Thryonomys swinderianus) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Spishi 2:
| ||||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.