Tennis
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tennis (pia tenisi) ni aina ya michezo inayotekelezwa na watu wawili au wanne wakishindana kwa kupiga mpira mdogo kwa raketi kwenye uwanja wa tennis. Shabaha ni kupiga mpira kwa upande wa mpinzani kwa namna inayomshinda kurudisha mpira. Akishindwa kurudisha mpira upande mwingine mpiganaji wa kwanza anashika pointi moja.
Wanaoshindana ni ama wanaume au wanawake, au timu za mwanaume mmoja na mwanamke mmoja.