Shingo ya nchi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Shingo ya nchi

Shingo ya nchi (ing./gir. isthmus) ni kanda nyembamba ya nchi kavu yenye maji kila upande inayounganisha sehemu mbili kubwa zaidi ya nchi.

Thumb
Shingo ya nchi ya Panama kati ya Amerika ya Kusini na Amerika ya Kati

Mfano bora ni shingo ya nchi ya Panama inayounganisha Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini. Mifano mengine mashihuri ni shingo ya nchi ya Suez baina Afrika (Misri) na Asia halafu shingo ya nchi ya Korintho kati ya rasi ya Peloponesi na Ugiriki bara.

Mara nyingi shingo ni mahali panapofaa kwa kujenga mfereji kwa sababu hapo umbali kati ya magimba mawili ya maji ni ndogo zaidi. Kwa hiyo shingo za nchi zilizotajwa juu huwa na mifereji yao:

Kwa namna ya kinyume shingo la nchi huligana na mlangobahari ambayo ni sehemu nyembamba ya bahari kati ya bara na kisiwa, kwa mfano mlango wa Gibraltar.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.