Sala
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sala (kutoka neno la Kiarabu صلاة, ṣalāh; pia maombi) ni njia ambayo binadamu anauelekea ulimwengu wa roho, hasa kwa nia ya kuongea na Mungu kwa sauti au kimoyomoyo.
Malengo yake yanaweza kuwa tofauti: kusifu, kushukuru, kuomba au kujiachilia.
Upande wa pili sala ni kutafakari ili kusikiliza na kuelewa ujumbe wa Mungu.
Sala inaweza kufanywa na mtu peke yake au na wengi pamoja, hata kwa kuimba.