From Wikipedia, the free encyclopedia
Pimbi, kwanga, perere au wibari ni wanyama wadogo wa familia Procaviidae. Jina la kwanga litumika kwa jenasi Heterohyrax na perere na wibari yatumika kwa jenasi Dendrohyrax. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara na Mashariki ya Kati, mara nyingi katika maeneo makavu na yenye miamba mingi. Spishi zote ni nene zenye mkia mfupi na manyoya mazito. Miguu yao ina vitakia vyenye ngozi nene na tezi nyingi za jasho ambavyo vinawasaidia kupanda miamba na miti. Rangi yao ni kijivu, kahawia au hudhurungi. Hula majani ya manyasi, ya mimea na ya miti.
Pimbi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Pimbi mkubwa kwenye Mlima Kenya (Procavia capensis) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 3, spishi 4:
| ||||||||||||||
Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.