Pigo la kona
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pigo la kona ni aina ya uanzishaji wa mpira uliokufa baada ya mpira kutoka nje ya uwanja kwa kuvuka mstari wa upande wa goli bila ya goli kufungwa na mpira huo kuwa umeguswa na mchezaji wa timu inayokaba. Mpira hupigwa kwa kutengwa kwenye kona ya uwanja, mahali mstari wa pembeni unapokutana na mstari wa upande wa goli. Mara kadhaa upigaji wa kona huweza kusababisha goli lakini ni nadra kulinganisha na penalti au faulu zinazopigwa karibu na eneo la penalti.