Noti ya benki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kwa maana nyingine ya neno hili tazama noti (maana)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d9/Jiao_zi.jpg/300px-Jiao_zi.jpg)
Noti ya benki, kifupi: noti, (kutoka Kiingereza "banknote") kwa kawaida ni kipande cha karatasi (pia: plastiki) kinachochapishwa na kuonyesha namba fulani na jina la pesa ya nchi fulani. Inakubaliwa kama njia ya malipo halali. Pamoja na sarafu ni pesa taslimu ya nchi fulani.
Kwa kawaida vipande vya sarafu au pesa taslimu metalia huwa na viwango vidogo zaidi na noti huwa na viwango vikubwa zaidi.