![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7c/Backyard_limes.jpg/640px-Backyard_limes.jpg&w=640&q=50)
Ndimu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ndimu ni tunda la mndimu (Citrus aurantiifolia), mti wa familia ya michungwa (Rutaceae).
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7c/Backyard_limes.jpg/640px-Backyard_limes.jpg)
Umbo lake ni mduara wenye rangi ya kijani mpaka njano, na kipenyo cha sm 3-6.
Lina ladha ya uchachu kwa sababu ya asidi ndani yake. Ndimu mara nyingi hutumika kuongeza ladha kwenye chakula na vinywaji. Kwa kawaida ni dogo kuliko limau, na chanzo kizuri pia cha vitamini C.
Katika kanda za tropiki na nusutropiki mindimu inaweza kumea mwaka wote maji yakiwapo. Ndimu huweza kuwa chungu au tamu. Ndimu chungu huwa na kiasi kikubwa cha sukari na asili ya asidi citric kuliko malimao na kuwa na ladha ya asili huku ndimu tamu hukosa asidi ndani yake hivyo kuwa na ladha tamu kwelikweli.
Ndimu ni matunda madogo, ambayo ngozi na nyama yake ni kati ya inchi moja au mbili hivi.