From Wikipedia, the free encyclopedia
Mbadili jinsia (pia Jinsia mkato; kwa Kiingereza: Transgender) ni mtu ambaye hujisikia, hujifikiria na kujiona au kujiigiza tofauti na jinsia yake ya kuzaliwa nayo [1].
Watu wa namna hiyo huona kwamba jinsia waliyozaliwa nayo si sahihi, hivyo wanataka kutambulika katika jamii vile wanavyojisikia, kwa mfano waweze kutumia vyoo vya jinsia wanayoipenda, kushiriki michezo ya jinsia wanayotaka [2] na kufungwa gerezani pamoja na watu wa jinsia wanayojisikia ingawa sivyo walivyo[3][4]. Baadhi ya nchi zimewakubalia, lakini wananchi wengi wameona si sawa wenye mwili wa kiume washindane na wanawake katika michezo kwa sababu kwao ni rahisi sana kupata ushindi; vilevile gerezani zimetokea kesi kadhaa za ubakaji dhidi ya wanawake halisi waliomo [5][6].
Pia kuna wale wanaoitwa kwa Kiingereza Transsexual: hawa ni miongoni mwa watu waliozaliwa na jinsia ya kiume wakataka wafanyiwe upasuaji ili wawe kama wanawake au kinyume chake. Mara nyingi wanaume ndio hutaka kuwa na viungo kama vya kike[7]. Hata hivyo hadi sasa jinsia haiwezi kubadilishwa. Matumizi ya mfululizo ya homoni na upasuaji katika viungo vya uzazi unaishia upande wa nje bila kubadili wala kuathiri DNA ya mhusika [8][9][10].
Wabadili jinsia huwa wanafariki dunia mapema kuliko watu wengine [11], pengine kwa kujiua [12], ama kwa sababu ya kubaguliwa katika baadhi ya mazingira [13][14][15][16], ama kwa sababu nyingine [17][18][19][20][21][22].
Tafiti mbalimbali zimeonyesha watu hao wana matatizo makubwa ya kiakili [23] [24][25] na nyingine zinasema kuchanganya watoto kuhusu jinsia kunaongeza matatizo yao na hivyo kuzidisha kesi za kujiua [26][27], hasa baada ya kutenganishwa na familia zao [28].
Kadiri wasenge wanavyoongezeka[29], wanazidi kupatikana pia wanaojuta hatua walizochukua kujibadilisha [30][31][32][33] na wanaolaumu waliowashauri vibaya [34][35][36][37][38][39], hasa waliopewa haraka [40][41][42][43] dawa za kuzuia ubalehe[44][45] na hatimaye kufanyiwa upasuaji [46][47] kabla hajaweza kuelewa matokeo yake [48][49][50][51] bila kuzingatia njia mbadala[52].
Kwa mujibu wa jumla ya tafiti zilizopima majuto hayo, asilimia 1 ya wabadili jinsia wa Marekani wanajuta kubadili jinsia[53]. Asilimia 10 za wabadili jinsia wa Marekani waliacha kubadili jinsia.[54][55] Miongoni mwa wale walioacha, asilimia 62 walirudia kubadili jinsia na baadaye wakaibadili tena.[54] Sababu zao za kuacha kujibadilisha ni mbalimbali, lakini ya kawaida sana ni hofu ya ubaguzi na kukanwa na jamii.[55]
Baadhi ya waliojuta wamefungua kesi dhidi ya waliowaelekeza [56][57][58][59][60], hasa baada ya kuona ugumu mkubwa wa kurudia hali asili (jambo ambalo pengine haliwezekani kabisa, hasa upande wa uzazi) [61][62][63]. Vilevile baadhi ya wazazi wao[64]
Hatua zao hizo, pamoja na hoja za wataalamu mbalimbali zinazoeleza madhara ya dawa hizo kwa watoto [65][66], zimelazimisha wenye mamlaka katika nchi mbalimbali kuchukua uamuzi wa kusimamisha mchakato wa namna hiyo [67][68][69][70][71][72][73][74][75][76][77][78][79]. Dawa hizo zimeboresha afya ya akili ya wabadili jinsia wengi[80], lakini zinaweza kuwa na athari mbaya kwa wengine.[81]
Baadhi wanalaumu uhamasishaji wa ushoga katika jamii [82][83][84][85][86][87][88] ambao pengine unalenga faida kubwa ya kiuchumi[89].
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.