Mnara wa taa nchini Misri, ulijengwa karne ya 3 na kuharibiwa Zama za kati From Wikipedia, the free encyclopedia
Mnara wa taa wa Aleksandria (pia hujulikana kama Pharos ya Aleksandria) ulikuwa mnara wa taa mjini Aleksandria huko Misri ambao ulihesabiwa kati ya maajabu saba ya dunia. Kimo chake hakijulikani kikamilifu lakini kilikuwa kati ya mita 110 na 150.
Mnara huo ulijengwa kwenye kisiwa kidogo kilichoitwa "Pharos" kilichokuwa mita chache mbele ya mwambao wa Aleksandria. Baadae mnara uliitwa kwa jina la kisiwa.
Ujenzi ulitokea wakati wa utawala wa Ptolemaio II Filadelfo (280-247 KK)[1] ambapo unakadiriwa kuwa angalau ni mita 100 za urefu wa jumla.[2]. Kwa karne nyingi Pharos ilikuwa kati ya majengo marefu ya dunia. Iliporomoka baada ya matetemeko ya ardhi yaliyotokea Aleksandria miaka 1303 na 1323.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.