Mkondo wa Benguela
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mkondo wa Benguela ni mkondo wa bahari katika Atlantiki ya Kusini unaotoka katika bahari baridi karibu na Antaktika na kuelekea kaskazini ukipita kwenye pwani la magharibi la Afrika. Mkondo una upana wa 200-3000 km.
mikondo baridi kwa rangi ya buluu - mikondo ya vuguvugu kwa rangi nyekundu
Mkondo husukuma maji baridi kwenye pwani la Afrika Kusini, Namibia na Angola. Maji yake huwa vuguvugu kiasi jinsi inavyofika kaskazini katika halijoto ya juu zaidi. Karibu na ikweta unabadilika mwelekeo wake na kuingia katika mkondo wa kusini ya ikweta. Sehemu ya maji yake inaingia katika bahari ya Karibi na kulisha mkondo wa ghuba.
Kusini ya rasi ya Afrika mkondo wa Benguela unakutana na maji ya vuguvugu ya mkondo wa Agulhas kutoka Bahari Hindi.