Kitongoji duni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kitongoji duni (pia: mtaa wa vibanda; kwa Kiingereza slum) ni mtaa jijini ambao mara nyingi huwa na nyumba duni zilizosimikwa karibu, miundomsingi duni na wakazi maskini.
Huduma za usambazaji wa maji safi, umeme na usalama huwa adimu. Vitongoji duni mara nyingi hupatikana mijini katika nchi zinazokua kimaendeleo kwa sababu ya kiwango kikuu cha ukuaji na uhamiaji.[1]