Musuli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Misuli [1] ni sehemu ya mwili wa wanyama na binadamu inayowezesha mwendo wa viungo vyake. misuli inaundwa na tishu ya pekee yenye uwezo wa kujinywea na kulegea. Wakati wa kujinywea huwa mifupi zaidi. Kwa njia hii misuli inayounganishwa na mifupa ya mkono au mguu huleta mwendo wa viungo hivi.