Milki ya Gupta
From Wikipedia, the free encyclopedia
Milki ya Gupta (kwa Kisanskrit: गुप्तसाम्राज्य, gupta sāmrājya) ilikuwa dola la kihistoria nchini Uhindi uliotawala sehemu kubwa ya Bara Hindi kati ya 320 - 550 BK na kutawaliwa na nasaba ya Gupta.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fb/SamudraguptaCoin.jpg/640px-SamudraguptaCoin.jpg)
Kipindi cha Gupta kilikuwa kipindi cha amani na maendeleo katika sayansi na sanaa. Wahindi wengi wanakitazama kuwa "enzi ya dhahabu" katika historia yao. Ustaarabu wa Uhindi uliweza kuongeza elimu na wezo wake katika fani nyingi kama vile sayansi, tekinolijia, uhandisi, sanaa, falsafa, hisabati, astronomia na dini zilizoendelea kuwa msingi wa utamaduni wa Kihindi.
Milki hii kubwa iliporomoka polepole kutokana na mafarakano ya ndani na uvamizi wa makabila ya Wahunni kutoka Asia ya Kati.