![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/50/Escudo_de_la_ciudad_de_M%25C3%25A9xico.svg/langsw-640px-Escudo_de_la_ciudad_de_M%25C3%25A9xico.svg.png&w=640&q=50)
Mexico (mji)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jiji la Mexico (kwa Kihispania: Ciudad de México) ni mji mkuu pia mji mkubwa wa nchi ya Mexico. Jiji lina wilaya 16, ambazo kila moja zimegawanywa katika vitongoji au colonias.
Jiji la Mexico | |
Mahali pa mji wa Mexico katika Mexico |
|
Majiranukta: 19°26′0″N 99°8′0″W | |
Nchi | Mexiko |
---|---|
Tovuti: http://www.df.gob.mx/ |
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/15/Montaje.Ciudad_de_M%C3%A9xico.jpg/640px-Montaje.Ciudad_de_M%C3%A9xico.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/50/Escudo_de_la_ciudad_de_M%C3%A9xico.svg/320px-Escudo_de_la_ciudad_de_M%C3%A9xico.svg.png)
Uko kwenye nyanda za juu za Mexico kwenye kimo cha m 2000 juu ya UB katika bonde refu linalopakana na milima mirefu. Kati ya milima hii ni volkeno za Popocatepetl na Iztaccihuatl na nyororo ya Sierra Nevada.
Mji wa Mexico ni pia mkoa wa kujitegemea, huitwa mara nyingi na Wamexiko wenyewe "Mexico DF" au kwa kifupi "DF" (DF = Distrito Federal, Mkoa wa Shirikisho), lakini tangu mwaka 2016 unaelekea kujitegemea zaidi kiutawala.
Idadi ya wakazi ni milioni 9, lakini pamoja na mitaa ya karibu idadi inafikia karibu milioni 20.4. Ni kati ya miji mikubwa kabisa duniani.