Mnururisho sumakuumeme (ing. electromagnetic radiation / electromagnetic waves) ni mnururisho wa mawimbi zinazounganisha uga sumaku na uga wa umeme na kubeba nishati. Mifano ya mawimbi sumakuumeme ni wimbiredio, mikrowevu, mawimbi ya joto, mawimbi ya urujuanimno, eksirei, na nuru inayoonekana kwetu.

Thumb
Spektra ya mawimbi sumakuumeme; nuru ni sehemu ya wawimbi haya

Tofauti na mawimbi ya mata kama wimbisauti zile za sumakumeme hazihitaji midia kwa uenezi wao. Zinaenea pia katika ombwe kwa kasi ya nuru.

Mawimbi yenye masafa (wavelength) mafupi ni mnururisho wa kuioniza na hivyo hatari kwa viumbehai kuanzia kiwango fulani, hasa gammarei na eksirei. Hata mnururisho wa urujuanimno ina hatari unaweza kusababisha mbabuko wa jua (ing. sunburn) kwenye ngozi ha hata kansa.

Pande mbalimbali za spektra ya sumakuumeme zinatofautiana kwa masafa ya mawimbi (wavelenghth), marudio (frequency) na kiwango cha nishati zinazosafirisha.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.