Mana
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mana (kwa Kiebrania מָן) ni chakula kilichotumiwa na Waisraeli walipotangatanga katika jangwa la Sinai miaka 40 mfululizo baada ya kutolewa na Musa nchini Misri walipokuwa wananyanyaswa.
Habari hizo zinapatikana katika vitabu vingi vya Biblia (hasa Kutoka 16:1-36 na Hesabu 11:1-9) na vilevile katika Kurani 5:27.
Pamoja na maelezo mbalimbali yaliyotolewa na wataalamu kuhusu asili ya chakula hicho, kwa imani kilitazamwa kama ishara ya pekee ya Mungu kuwashughulikia watu wake.
Yesu alikitumia hicho pia kujitambulisha ni nani kwa binadamu wote: "Mimi ndimi chakula cha kweli kilichoshuka kutoka mbinguni" (Yoh 6).