![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0a/Flickr_-_Rainbirder_-_Black-winged_Red_Bishop_%2528Euplectes_hordeaceus%2529.jpg/640px-Flickr_-_Rainbirder_-_Black-winged_Red_Bishop_%2528Euplectes_hordeaceus%2529.jpg&w=640&q=50)
Kweche
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kweche ni ndege wadogo wa jenasi Euplectes katika familia Ploceidae ambao wanatokea Afrika. Kuna makundi mawili ya kweche. Ndege wa kundi moja (bishops) ni wadogo kwa kulinganisha na madume wana mkia mfupi wakati wa kuzaa. Wakati huo rangi za madume ni nyeusi na nyekundu, machungwa au njano. Ndege wa kundi jingine (widowbirds) ni wakubwa zaidi na madume wana mkia mrefu wakati wa kuzaa. Wakati huo rangi za madume ni nyeusi kwa kiasi kikubwa pamoja na sehemu zenye rangi nyingi kama nyeupe, nyekundu na njano.
Kweche | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Kweche mtama | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Spishi 17:
| ||||||||||||||
Ndege hawa hula mbegu hasa lakini wadudu pia, hususa makinda. Hulifuma tago lao kwa manyasi katikati ya matete. Matago yao hupatikana katika makundi. Dume hufanya mruko wa kukoga ili kubembeleza jike akitimua manyoya yake (bishops) au akitandaza mkia wake (widowbirds). Jike huyataga mayai 2-4.