Krisma
From Wikipedia, the free encyclopedia
Krisma (kutoka Kigiriki: χρῖσμα, Khrisma, yaani mpako) ni mafuta ya kunukia yanayotumiwa na Wakristo wa madhehebu mbalimbali (Wakatoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Wakatoliki wa Kale, Waanglikana, Wamormoni na baadhi ya Walutheri) katika ibada kadhaa, hasa sakramenti za ubatizo, kipaimara na daraja takatifu.
Krisma ndiyo asili ya majina Kristo, Wakristo yanayomtambulisha Yesu na wafuasi wake.