Kofi Annan
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kofi Atta Annan (8 Aprili 1938 - 18 Agosti 2018) alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa 1996 - 2006. Annan na Umoja wa Mataifa walipata Tuzo ya Amani ya Nobeli mwaka 2001. Alikuwa mwanzilishi na mwenyekiti wa Kofi Annan Foundation na pia mwenyekiti wa Elders, shirika la kimataifa lililoanzishwa na Nelson Mandela.