![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f0/Long_shadows_on_Lammer_Law_-_geograph.org.uk_-_90304.jpg/640px-Long_shadows_on_Lammer_Law_-_geograph.org.uk_-_90304.jpg&w=640&q=50)
Kivuli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kivuli ni eneo lenye nuru kidogo katika mazingira yenye nuru zaidi. Kinapatikana nyuma ya gimba kinachoangazwa upande moja lakini kinazuia nuru kuendelea na hivyo kuunda eneo lenye giza au nuru kidogo nyuma yake.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f0/Long_shadows_on_Lammer_Law_-_geograph.org.uk_-_90304.jpg/320px-Long_shadows_on_Lammer_Law_-_geograph.org.uk_-_90304.jpg)
Kila kitu kisichopitisha nuru ndani chake kinaweza kuwa na kivuli kikianganzwa upande mmoja. Mfano wa gimba ambalo halina kivuli ni hewa au pia kioo safi dirishani.
Kwa maana pana zaidi kuna pia kivuli cha mnururisho usio nuru ya kuona kwa macho; mata ogania ndani ya mwili unapitisha au kuzuia mnururisho wa eksirei kwa viwango tofauti na kuonekana baadaye kwenye picha kwa rangi tofauti kutokana na "kivuli" dhidi ya mionzi hii.