From Wikipedia, the free encyclopedia
Viseleagofu ni ndege wa jenasi Jynx, jenasi pekee ya nusufamilia Jynginae katika familia Picidae. Wanafanana na vigong'ota wadogo lakini domo lao ni dugi na fupi zaidi. Kwa hivyo hutafuta wadudu na mabuu katika miti na matawi yanayooza au ardhini; hula chungu, samesame na siafu hasa.
Kiseleagofu | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kiseleagofu koo-jekundu | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ndege hawa wana rangi ya kamafleji: nyeupe, kijivu na kahawia; manyoya yao yamechorwa kwa milia myembamba mingi iliyo myeusi. Wakitishwa wanaweza kulinyoosha koo lao na kukigeuza kichwa chao takriban nyuzi 180 kwa kila upande, wakati huo huo hufanya sauti ya sss kama nyoka. Jike huyataga mayai 7-9 katika tundu la kigong'ota.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.