Kikirgizi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kikirgizi ni lugha ya Kiturki nchini Kirgizia, Uchina, Afghanistan, Urusi, Uturuki na Uzbekistan inayozungumzwa na Wakirgizi. Kikirgizi ni lugha rasmi katika nchi za Kirgizia. Mwaka wa 2009 idadi ya wasemaji wa Kikirgizi nchini Kirgizistan imehesabiwa kuwa watu 3,830,000. Pia kuna wasemaji 160,000 nchini Uchina (2000), 60,100 nchini Tajikistan (2012) na 750 nchini Afghanistan (2000). Idadi za wasemaji wa Kikirgizi nchini Uturuki, Uzbekistan na Urusi hazijulikani. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kikirgizi iko katika kundi la Kiturki ya Magharibi.