Kanuni ya Mt. Benedikto
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kanuni ya Mtakatifu Benedikto ni kati ya maandishi kwa ajili ya utawa yaliyoathiri zaidi historia ya Kanisa na ya ulimwengu kwa jumla, hasa Ulaya, kwa kuwa baada ya muda mfupi ilikuja kuongoza maisha ya wamonaki karibu wote wa Kanisa la magharibi.
Iliandikwa na Benedikto wa Nursia kwa kutumia kanuni za kitawa zilizotangulia, hasa Kanuni ya mwalimu, pamoja na mang'amuzi yake yaliyojaa busara.