Kanisa kuu ni jina la heshima la jengo la ibada la madhehebu mbalimbali ya Ukristo ambalo Askofu wa jimbo (dayosisi) fulani analitumia kwa kawaida kutekeleza kazi yake kama mchungaji mkuu wa waamini wake, kama vile kuhubiri na kufundisha Neno la Mungu, kutakasa watu kwa sakramenti na sala mbalimbali na kuwaunganisha wote katika kumfuata Yesu pamoja.

Thumb
Upande wa mbele wa Basilika kuu la Mt. Yohane huko Laterano wakati wa usiku. Ndilo kanisa kuu la Roma. Juu ya paa, pamoja na nyingine, kuna sanamu ya Yesu Mkombozi tena 12 za Mitume wa Yesu.
Thumb
Kanisa kuu la Kilutheri la Helsinki, Ufini.
Thumb
Kanisa kuu la Kikatoliki huko Salta, Argentina.

Jina

Jina hilo linashuhudiwa tayari na maandishi ya mwaka 516.

Linaitwa pia "kanisa mama" kwa sababu ni kama mama wa makanisa yote ya jimbo hilo.

Upekee

Ndani yake umo ukulu, yaani kiti cha Askofu kisichopatikana katika makanisa mengine.

Kanisa kuu la Wakatoliki wote

Kwa kuwa imani ya Kanisa Katoliki ni kwamba Papa wa Roma ni mkuu wa maaskofu wote duniani, kanisa kuu la jimbo lake ni pia kanisa kuu la Wakatoliki wote. Ndiyo sababu mlangoni mwa basilika kuu la Laterano imeandikwa kwamba ndilo "kichwa na mama wa makanisa yote ya jiji na ya dunia nzima".

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kanisa kuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.