Malaika Gabrieli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Malaika Gabrieli (kwa Kiebrania גַּבְרִיאֵל, Gavri'el, Gaḇrîʼēl, Mungu ni nguvu yangu; kwa Kiarabu جبريل, Jibrīl au جبرائيل Jibrāʾīl) ni malaika aliyetumwa na Mungu kuleta ujumbe wa pekee[1] katika dini zinazotaka kufuata imani ya Abrahamu.
Kwa sababu hiyo Wakatoliki, kuanzia Pseudodionisi na Papa Gregori I, wanamheshimu kama malaika mkuu pamoja na malaika Mikaeli na malaika Rafaeli, hasa tarehe 29 Septemba[2][3].
Wakristo wengine pia wanamheshimu kwa kupasha habari ya kutungwa mimba kwa Yohane Mbatizaji[4], halafu kwa Yesu[5] inavyosimuliwa na Injili ya Luka.
Waislamu pia wanamheshimu kwa ajili hiyo na kwa kumletea Mtume Muhammad ufunuo wa Kurani.
Kwa mara ya kwanza jina lake liliandikwa katika kitabu cha Danieli (8:15-26; 9:21-27).