From Wikipedia, the free encyclopedia
Hifadhi ya Taifa ya Nairobi ilikuwa mbuga ya kwanza nchini Kenya ilipoanzishwa mwaka wa 1946. Iko takriban kilomita 7 kusini mwa katikati ya Nairobi, mji mkuu wa Kenya, na ni ndogo ikilinganishwa na mbuga nyingine za wanyama barani Afrika. Majumba marefu jijini Nairobi yaweza kuonekana kutoka kwenye mbuga.
Mbuga hii ina wanyamapori wengi tofauti.[1] Ni ugo tu unaotenganisha mbuga hii ya wanyama kutoka mji mkuu.[2] Wanyama walao mimea hujaa sana katika mbuga hii wakati wa kiangazi. Ni mojawapo kati ya makimbilio ya vifaru yaliyofanikiwa sana nchini Kenya.
Kwamba mbuga hii ipo karibu na jiji la Nairobi husababisha mgogoro baina ya wanyama na wananchi na pia hutishia uhamaji wa wanyama.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.