Wazamaji (tafsiri kutoka Kiing.: diver) ni ndege wa maji wa jenasi Gavia, jenasi pekee ya familia Gaviidae. Wanafanana na vibisi na minandi lakini ni tofauti na wamepewa oda yao Gaviiformes. Wana ngozi kati ya vidole kama minandi lakini domo lao lina ncha kali bila kulabu kama vibisi. Kama zile spishi nyingine huzamia kabisa ili kukamata samaki, gegereka, amfibia, koa na luba. Hulijenga tago lao kwa matope, mimea ya maji na manyasi ardhini karibu na maji ya ziwa katika kande za kaskazini za Amerika, Ulaya na Asia. Jike huyataga mayai 1-3. Nje ya majira ya kuzaa hupatikana baharini na spishi kadhaa huhama mpaka pwani za Afrika ya Kaskazini-magharibi.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Mzamaji
Thumb
Mzamaji koo-jeusi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Gaviiformes (Ndege kama wazamaji)
Familia: Gaviidae (Wazamaji)
Jenasi: Gavia
Forster, 1788
Spishi: G. adamsii (Gray, 1859)

G. arctica Linnaeus, 1758
G. immer (Brünnich, 1764)
G. pacifica (Lawrence, 1858)
G. stellata (Pontoppidan, 1763)

Funga

Spishi za Afrika

Spishi za mabara mengine

Picha

Makala hii kuhusu "Mzamaji (ndege)" inatumia neno (au maneno) ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio la kutafsiri neno (au maneno) la asili diver kutoka lugha ya Kiingereza. Neno (au maneno) la jaribio ni mzamaji.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.