Jenasi ya ndege wa maji wanaozama From Wikipedia, the free encyclopedia
Wazamaji (tafsiri kutoka Kiing.: diver) ni ndege wa maji wa jenasi Gavia, jenasi pekee ya familia Gaviidae. Wanafanana na vibisi na minandi lakini ni tofauti na wamepewa oda yao Gaviiformes. Wana ngozi kati ya vidole kama minandi lakini domo lao lina ncha kali bila kulabu kama vibisi. Kama zile spishi nyingine huzamia kabisa ili kukamata samaki, gegereka, amfibia, koa na luba. Hulijenga tago lao kwa matope, mimea ya maji na manyasi ardhini karibu na maji ya ziwa katika kande za kaskazini za Amerika, Ulaya na Asia. Jike huyataga mayai 1-3. Nje ya majira ya kuzaa hupatikana baharini na spishi kadhaa huhama mpaka pwani za Afrika ya Kaskazini-magharibi.
Mzamaji | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mzamaji koo-jeusi | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.