Ndege wa familia Calyptomenidae From Wikipedia, the free encyclopedia
Vijogoo-shamba au bandabanda ni ndege wa familia Calyptomenidae. Zamani ndege hawa waliainishwa katika familia Eurylaimidae lakini siku hizi inabaki spishi moja tu ndani yake, kijogoo-shamba kijani.
Kijogoo-shamba | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kijogoo-shamba utosi-mweusi | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 2, spishi 6 + 1 kutoka familia nyingine:
| ||||||||||||||
Wana domo pana na spishi za Asia pamoja na kijogoo-shamba kijani zina rangi ya majani lakini spishi nyingine za Afrika ni kahawia na nyeupe zenye michirizi myeusi. Ndege hawa wanatokea misitu mizito. Hula matunda na hukamata wadudu kwa namna ya shore au chechele. Hupenda kuwa kwa makundi ya hadi kufikia ndege 20. Tago la vijogoo-shamba ni mjengo mkubwa (mpaka nusu mita) unaofungika na wenye mwingilio kwa upande wake. Limefumika kwa vitawi, manyasi na majani na kufunikika kwa tando za buibui, vigoga na kuvumwani. Jike huyataga mayai 1-3.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.