Delta ya barani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Delta ya barani ni eneo nchini na mbali na bahari ambapo mto unapanuka kwa umbo la delta.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/45/DeltaOkawango.jpg/640px-DeltaOkawango.jpg)
Kupanuka huku kunatokea kama mto unafika penye mtelemko mdogo kama tambarare au beseni. Kutokana na uhaba wa mtelemko kasi ya maji inapungua na mashapo yanatelemka chini yakijenga vizuizi na kusababisha kugawanyikiwa kwa mto kuwa na mikono mbalimbali.
Tofauti na delta ya mto baharini au ziwani delta ya aina hii hutokea barani kabisa.