Biashara ya ng'ambo ya Sahara
From Wikipedia, the free encyclopedia
Biashara ya ng'ambo ya Sahara (vilevile Biashara ya Masafa Marefu ya Afrika ya Magharibi) ilikuwa biashara iliyohusisha Afrika ya Magharibi na Afrika ya Kaskazini kupitia jangwa la Sahara.
Biashara hiyo ni mfano mzuri wa biashara za kanda au masafa marefu ambayo yaliongozwa katika upande wa Afrika Magharibi.
Biashara hiyo ilianza mnamo karne ya 4 na iliendelea zaidi hadi katika karne ya 17 ambapo ilianguka mazima.
Biashara ilikuwa na matokeo kadha wa kadha katika historia ya Afrika Magharibi na ya Afrika kwa ujumla.