From Wikipedia, the free encyclopedia
Mabata mkia-ngumu ni ndege wa maji wa nusufamilia Oxyurinae katika familia Anatidae. Manyoya ya mkia wao ni makavu na yametandawaa mara nyingi. Rangi ya dume ni kahawia au kahawiachekundu na domo lake lililovimba msingini ni buluu; jike ni mweusi au kijivu wenye domo la rangi ile ile. Spishi hizi huzamia kabisa ili kutafuta chakula. Hula mimea na invertebrata ya maji. Miguu yao iko nyuma sana, kama ile ya mabata wazamaji, ili kujisogeza mbele vizuri ndani ya maji. Kwa sababu hiyo hawawezi kutembea vizuri. Hujenga tago lao ndani ya uoto mzito wa maji. Jike huyataga mayai 3-8, lakini pengine hadi mayai 12 yanapatikana kwa sababu jike mwingine ameongezea mayai yake.
Bata mkia-ngumu | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Bata kichwa-cheupe | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 4, spishi 10:
| ||||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.